Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 115

115
Zaburi 115
Mungu Mmoja Wa Kweli
1 Sio kwetu sisi, Ee Bwana, sio kwetu sisi,
bali utukufu ni kwa jina lako,
kwa sababu ya upendo
na uaminifu wako.
2 Kwa nini mataifa waseme,
“Yuko wapi Mungu wao?”
3 Mungu wetu yuko mbinguni,
naye hufanya lolote limpendezalo.
4 Lakini sanamu zao ni za fedha na dhahabu,
zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
5 Zina vinywa, lakini haziwezi kusema,
zina macho, lakini haziwezi kuona;
6zina masikio, lakini haziwezi kusikia,
zina pua, lakini haziwezi kunusa;
7zina mikono, lakini haziwezi kupapasa,
zina miguu, lakini haziwezi kutembea;
wala koo zao haziwezi kutoa sauti.
8 Wale wanaozitengeneza watafanana nazo,
vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
9 Ee nyumba ya Israeli, mtumainini Bwana,
yeye ni msaada na ngao yao.
10 Ee nyumba ya Aroni, mtumainini Bwana,
yeye ni msaada na ngao yao.
11 Ninyi mnaomcha, mtumainini Bwana,
yeye ni msaada na ngao yao.
12 Bwana anatukumbuka na atatubariki:
ataibariki nyumba ya Israeli,
ataibariki nyumba ya Aroni,
13 atawabariki wale wanaomcha Bwana,
wadogo kwa wakubwa.
14 Bwana na awawezeshe kuongezeka,
ninyi na watoto wenu.
15 Mbarikiwe na Bwana
Muumba wa mbingu na dunia.
16 Mbingu zilizo juu sana ni mali ya Bwana,
lakini dunia amempa mwanadamu.
17 Sio wafu wanaomsifu Bwana,
wale washukao mahali pa kimya,#115:17 Mahali pa kimya maana yake ni Kuzimu, yaani Sheol kwa Kiebrania.
18 bali ni sisi tunaomtukuza Bwana,
sasa na hata milele.
Msifuni Bwana.#115:18 Msifuni Bwana ni Kiebrania Hallelu Yah.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 115: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha