Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Luka 13:18-21

Luka 13:18-21 NEN

Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaufananisha na nini? Umefanana na punje ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake. Nayo ikakua, ikawa mti nao ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.” Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha Ufalme wa Mungu na nini? Unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Luka 13:18-21