Kumbukumbu 1:26-33
Kumbukumbu 1:26-33 NENO
Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Mkanung’unika ndani ya mahema yenu na kusema, “Mwenyezi Mungu anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza. Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’ ” Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope. Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa, na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea hadi mkafika mahali hapa.” Pamoja na hili, hamkumtegemea Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonesha njia mtakayoiendea.