Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Wakolosai 4:2-6

Wakolosai 4:2-6 NENO

Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru. Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena neno lake, ili tupate kuitangaza siri ya Al-Masihi, ambayo kwa ajili yake nimefungwa. Ombeni ili nipate kuitangaza hiyo siri kwa udhahiri kama inipasavyo. Nendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Maneno yenu yawe yamejaa neema siku zote, yanayofaa, ili mjue jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.