Kisha Anania akaondoka, akaenda, akaingia nyumbani mle, akambandikia mikono akisema: Ndugu yangu Sauli, Bwana Yesu aliyekuotokea njiani, alipokuja, amenituma, upate kuona tena na kujazwa Roho takatifu. Papo hapo pakawa kama magamba yaliyoanguka toka machoni pake, akaona, tena akainuka, akabatizwa.