1
Yakobo 1:2-3
Swahili Revised Union Version
Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
Linganisha
Chunguza Yakobo 1:2-3
2
Yakobo 1:5
Lakini mmoja wenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
Chunguza Yakobo 1:5
3
Yakobo 1:19
Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika
Chunguza Yakobo 1:19
4
Yakobo 1:4
Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.
Chunguza Yakobo 1:4
5
Yakobo 1:22
Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu.
Chunguza Yakobo 1:22
6
Yakobo 1:12
Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji la uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.
Chunguza Yakobo 1:12
7
Yakobo 1:17
Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.
Chunguza Yakobo 1:17
8
Yakobo 1:23-24
Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo.
Chunguza Yakobo 1:23-24
9
Yakobo 1:27
Dini iliyo safi, isiyo na dosari mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Chunguza Yakobo 1:27
10
Yakobo 1:13-14
Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
Chunguza Yakobo 1:13-14
11
Yakobo 1:9
Lakini ndugu asiye na cheo na afurahi kwa kuwa ametukuzwa
Chunguza Yakobo 1:9
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video