Mataifa mengi yatakuja na kusema,
“Njooni, twendeni kwenye mlima wa Mwenyezi Mungu,
kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.
Atatufundisha njia zake,
ili tuweze kuenenda katika mapito yake.”
Torati itatoka Sayuni,
neno la Mwenyezi Mungu litatoka Yerusalemu.