YouVersion Logo
Search Icon

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na MatendoSample

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

DAY 37 OF 40

Paulo anasimama mbele ya baraza la viongozi wa dini ili kujitetea. Baada ya kukatizwa na fujo na kufikiria kimakosa kuwa kuhani mkuu alikuwa mtu mwingine, Paulo anaona kuwa hali si nzuri na anajaribu kufikiria cha kufanya. Anaona kuwa baraza limegawanyika kwa madhehebu mawili ya kidini: Masadukayo na Mafarisayo. Masadukayo hawaamini kuhusu ufufuo au malaika, huku Mafarisayo wakifasiri sheria kwa shuruti zaidi na wana shauku kuhusu ufufuo na malaika ambavyo Masadukayo hukataa. Paulo anaona kugawanyika kati ya baraza kama fursa ya kuondoa umakinifu kwake, na anaanza kupiga kelele kuwa yeye ni Mfarisayo na ameshtakiwa kwa tumaini la kufufuka kwa waliokufa.

Kutokana na hili, mjadala mrefu unaanza. Hili linaonekana kufanikiwa kwanza, na hata Mafarisayo wanaanza kumtetea Paulo. Lakini baada ya muda mfupi, ubishi unakuwa mkali hadi maisha ya Paulo yanakuwa hatarini tena. Anaondolewa na kamanda wa Kirumi na kuwekwa kuzuizini kinyume na sheria. Usiku unaofuata, Yesu aliyefufuka anasimama kando ya Paulo ili kumtia moyo, akisema kuwa kwa kweli Paulo atatekeleza kusudi la Yesu ndani ya Rumi. Kwa hivyo asubuhi, wakati dada yale Paulo anapomtembelea ili kumwambia kuwa zaidi ya Wayahudi 40 wanapanga njama ya kumvamia na kumuua, Paulo ana neno kuu la faraja analotegemea kwa hifadhi. Uvamizi hautafaulu kukamilisha misheni ya Paulo. Ataishi kuona Roma, kama tu Yesu alivyosema angeiona. Kama ilivyotarajiwa, onyo linamfikia kamanda kwa muda ili kukatiza njama hiyo. Paulo anapelekwa Kaisaria na zaidi ya wanaume 400 waliofunzwa ili kuhakikisha kuwa anawasili salama.

Day 36Day 38

About this Plan

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo huwahimiza watu, vikundi vidogo, na familia kusoma vitabu vya Luka na Matendo ya Mitume kwa siku 40. Mpango huu unajumuisha video zilizohuishwa na mihtasari ili kuwasaidia washiriki kukutana na Yesu. Na kujifunza kutoka kwenye usanifu mwema wa kifasihi wa Luka na mtiririko wa mawazo.

More