YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 15

15
Rafiki ya Mungu
(Zaburi ya Daudi)
1Nani ee Mwenyezi-Mungu atakayekaa hemani mwako?
Nani atakayeishi juu ya mlima wako mtakatifu?
2Ni mtu aishiye bila lawama,
atendaye daima yaliyo mema,
asemaye ukweli kutoka moyoni;
3ni mtu asiyesengenya watu,
asiyemtendea uovu rafiki yake,
wala kumfitini jirani yake;
4ni mtu anayewadharau wafisadi,
lakini huwaheshimu wamchao Mwenyezi-Mungu;
ni mtu asiyegeuza kiapo chake hata kikimtia hasara;
5asiyekopesha fedha yake kwa riba,
wala kupokea rushwa kumdhulumu asiye na hatia.
Mtu atendaye hayo,
kamwe hatatikisika.

Currently Selected:

Zaburi 15: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in