YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 15

15
Rafiki ya Mungu
(Zaburi ya Daudi)
1Nani ee Mwenyezi-Mungu atakayekaa hemani mwako?
Nani atakayeishi juu ya mlima wako mtakatifu?
2Ni mtu aishiye bila lawama,
atendaye daima yaliyo mema,
asemaye ukweli kutoka moyoni;
3ni mtu asiyesengenya watu,
asiyemtendea uovu rafiki yake,
wala kumfitini jirani yake;
4ni mtu anayewadharau wafisadi,
lakini huwaheshimu wamchao Mwenyezi-Mungu;
ni mtu asiyegeuza kiapo chake hata kikimtia hasara;
5asiyekopesha fedha yake kwa riba,
wala kupokea rushwa kumdhulumu asiye na hatia.
Mtu atendaye hayo,
kamwe hatatikisika.

Currently Selected:

Zaburi 15: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy