YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 16

16
Kuomba usalama
(Utenzi wa Daudi)
1Unilinde ee Mungu;
maana kwako nakimbilia usalama.
2Namwambia Mungu: “Wewe u Bwana wangu;
sina jema lolote ila wewe.”
3Ni bora sana hao watakatifu walioko nchini,
kukaa nao ndiyo furaha yangu.#16:3 Ni bora … yangu: Au Na kuhusu miungu ya uongo humu nchini, mimi nilidhania kuwa ina nguvu.
4Lakini wanaoabudu miungu mingine,#16:4 Lakini … mengi: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
watapata mateso mengi.
Tambiko ya damu sitaitolea kamwe,
na majina ya miungu hiyo sitayataja.
5Wewe ee Mwenyezi-Mungu ndiwe riziki yangu kuu,
majaliwa yangu yamo mikononi mwako.
6Umenipimia sehemu nzuri sana;
naam, urithi wangu ni wa kupendeza.
7Namsifu Mwenyezi-Mungu kwa kuniongoza,
usiku dhamiri yangu yanionya.
8 # Taz Mate 2:25-28 Namweka Mwenyezi-Mungu mbele yangu daima;
yuko pamoja nami, wala sitatikisika.
9Kwa hiyo nitafurahi kwa moyo wote na kushangilia,
nami nitakaa salama salimini.
10 # Taz Mate 13:35 Naam wewe hutaiacha nafsi yangu kuzimu,
hutaniacha mimi mwaminifu wako nipate kuoza.
11Wanionesha njia ya kufikia uhai;
kuwako kwako kwanijaza furaha kamili,
katika mkono wako wa nguvu mna mema ya milele.

Currently Selected:

Zaburi 16: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy