YouVersion Logo
Search Icon

Zab 112

112
Baraka za Mwenye Haki
1Haleluya.
Heri mtu yule amchaye BWANA,
Apendezwaye sana na maagizo yake.
2Wazao wake watakuwa hodari duniani;
Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.
3 # Mit 3:16; 15:6; Isa 33:6; Mt 6:33; 2 Kor 6:10 Nyumbani mwake mna utajiri na mali,
Na haki yake yakaa milele.
4Nuru huwazukia wenye adili gizani;
Ana fadhili na huruma na haki.
5 # Lk 6:35 Heri atendaye fadhili na kukopesha;
Atengenezaye mambo yake kwa haki.
6Kwa maana hataondoshwa kamwe;
Mwenye haki atakumbukwa milele.
7Hataogopa habari mbaya;
Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.
8Moyo wake umethibitika hataogopa,
Hata awaone watesi wake wameshindwa.
9 # Lk 11:41; Rum 12:13; Mdo 4:35; 20:35; 2 Kor 8:9; 9:9; 1 Tim 6:18 Amekirimu, na kuwapa maskini,
Haki yake yakaa milele,
Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.
10 # Lk 13:28 Asiye haki ataona na kusikitika,
Atasaga meno yake na kuyeyuka,
Tamaa ya wasio haki itapotea.

Currently Selected:

Zab 112: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy