YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 113

113
Zaburi 113
Kumsifu Bwana Kwa Wema Wake
1 Msifuni Bwana.
Enyi watumishi wa Bwana msifuni,
lisifuni jina la Bwana.
2 Jina la Bwana na lisifiwe,
sasa na hata milele.
3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,
jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
4 Bwana ametukuka juu ya mataifa yote,
utukufu wake juu ya mbingu.
5 Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu,
Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
6 ambaye huinama atazame chini
aone mbingu na nchi?
7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,
na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
8 huwaketisha pamoja na wakuu,
pamoja na wakuu wa watu wake.
9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,
akiwa mama watoto mwenye furaha.
Msifuni Bwana.

Currently Selected:

Zaburi 113: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy