YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 114

114
Zaburi 114
Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri
1 Wakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3 Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

Currently Selected:

Zaburi 114: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy