Soma Biblia Kila Siku Juni/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Juni/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F31560%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Tuombapo, Mungu hutujalia upendo, busara na ujuzi sahihi wa mapenzi yake kwa njia ya Yesu Kristo. Tena twatakaswa na kujazwa matunda ya haki. Hata tukilazimika kuteswa kwa ajili ya Kristo, twajua atatukuzwa. Wengine waweza kushangilia mateso hayo, lakini hata katika mashangilio yao, Kristo atahubiriwa na kutukuzwa. Haidhuru kitu kama Kristo atahubiriwa kwa husuda au kwa wema. Furaha yetu Wakristo ni kwamba Kristo anahubiriwa.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Juni/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F31560%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabblia.or.tz/