Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku Julai 2021Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Julai 2021](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F26577%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Ni unabii kuhusu hukumu ya Mungu juu ya adui mkubwa wa mwisho wa Israeli. Majina ya “Gogu” na “Magogu” ni ya kimfano, na matokeo yote katika unabii yatatukia baada ya siku nyingi (m.8). Bado tunasubiri unabii huu kutimia, ila ujumbe wake ni wazi: Mungu ndiye mlinzi wa watu wake. Hakuna haja ya kuwaogopa wanaotujia kwa uovu tukiwa mkononi mwa Bwana. Hata wazo la kushambulia Israeli, ndiye Mungu aliyeliweka moyoni mwa adui huyo (m.16, Nawe utapanda juu uwajilie watu wangu, Israeli, kama wingu kuifunika nchi; itakuwa katika siku za mwisho, nitakuleta upigane na nchi yangu, ili mataifa wanijue, nitakapotakaswa kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao). Hivyo wote watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Julai 2021](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F26577%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Julai 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu k...
More
Tungependa kuishukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz