Zaburi 59:1-9
Zaburi 59:1-9 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu. Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamepanga kunishambulia; Ee BWANA, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu. Bila kosa langu wanaenda mbio, kujiweka tayari; Inuka utazame na kunisaidia. Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uinuke. Uwapatilize mataifa yote; Usimrehemu hata mmoja wa wale wapangao maovu kwa hila. Wakati wa jioni hurudi, wakilia kama mbwa, Na kuzungukazunguka mjini. Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye? Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote. Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu.
Zaburi 59:1-9 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu. Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamenikusanyikia; Ee BWANA, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu. Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari; Uamke uonane nami, na kutazama. Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uamke. Uwapatilize mataifa yote; Usiwarehemu waovu wafanyao uovu hata mmoja. Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa, Na kuzunguka-zunguka mjini. Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye? Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote. Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu
Zaburi 59:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)
Ee Mungu wangu, uniokoe na maadui zangu; unikinge na hao wanaonishambulia. Uniokoe na hao wanaotenda maovu; unisalimishe kutoka kwa hao wauaji! Tazama! Wananivizia waniue; watu wakatili wanachochea ugomvi dhidi yangu. Bila ya kosa, hatia au dhambi yangu, wanakimbia, ee Mwenyezi-Mungu, kujiweka tayari. Uinuke, ee Mwenyezi-Mungu, ukatazame na kunisaidia! Uinuke, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu Mwenye Nguvu, Mungu wa Israeli. Uamke, uwaadhibu hao watu wasiokujua; usiwaache hao wanaopanga ubaya. Kila jioni maadui hao hurudi wakibweka kama mbwa, na kuzungukazunguka mjini. Tazama, ni matusi tu yatokayo mdomoni mwao, maneno yao yanakata kama upanga mkali; tena wanafikiri hakuna anayewasikia. Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawacheka; unawapuuza hao watu wote wasiokujua. Nitakungoja, ewe uliye nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, u ngome yangu.
Zaburi 59:1-9 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu. Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamepanga kunishambulia; Ee BWANA, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu. Bila kosa langu wanaenda mbio, kujiweka tayari; Inuka utazame na kunisaidia. Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uinuke. Uwapatilize mataifa yote; Usimrehemu hata mmoja wa wale wapangao maovu kwa hila. Wakati wa jioni hurudi, wakilia kama mbwa, Na kuzungukazunguka mjini. Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye? Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote. Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu.
Zaburi 59:1-9 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Ee Mungu wangu, uniponye na adui zangu, Uniinue juu yao wanaoshindana nami. Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu. Kwa maana wanaiotea nafsi yangu; Wenye nguvu wamenikusanyikia; Ee BWANA, si kwa kosa langu, Wala si kwa hatia yangu. Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari; Uamke uonane nami, na kutazama. Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uamke. Uwapatilize mataifa yote; Usiwarehemu waovu wafanyao uovu hata mmoja. Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa, Na kuzunguka-zunguka mjini. Tazama, kwa vinywa vyao huteuka, Midomoni mwao mna panga, Kwa maana ni nani asikiaye? Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki mataifa yote. Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu
Zaburi 59:1-9 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)
Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu. Uniponye na watu watendao maovu, uniokoe kutokana na wanaomwaga damu. Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Mwenyezi Mungu, mimi sijakosea wala kutenda dhambi. Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya! Ee Mungu, Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, uliye Mungu wa Israeli, zinduka uyaadhibu mataifa yote; usioneshe huruma kwa wasaliti waovu. Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji. Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema panga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?” Lakini wewe, Mwenyezi Mungu, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote. Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu