Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Wimbo Ulio Bora 3

3
1Usiku nikiwa kitandani mwangu,
niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu;
nilimtafuta, lakini sikumpata.
2Niliamka nikazunguka mjini,
barabarani na hata vichochoroni,
nikimtafuta yule wangu wa moyo.
Nilimtafuta, lakini sikumpata.
3Walinzi wa mji waliniona
walipokuwa wanazunguka mjini.
Basi nikawauliza,
“Je, mmemwona mpenzi wangu wa moyo?”
4Mara tu nilipoachana nao,
nilimwona mpenzi wangu wa moyo;
nikamshika wala sikumwachia aondoke,
hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu,
hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.
5Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,
kama walivyo paa au swala,
msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,
hadi hapo wakati wake utakapofika.
Shairi la tatu
Bibi arusi
6Ni kitu gani kile kitokacho jangwani
kama mnara wa moshi,
kinukiacho manemane na ubani,
manukato yauzwayo na wafanyabiashara?
7Tazama! Ni machela ya Solomoni;
amebebwa juu ya kiti chake cha enzi;
amezungukwa na walinzi sitini,
mashujaa bora wa Israeli.
8Kila mmoja wao ameshika upanga,
kila mmoja wao ni hodari wa vita.
Kila mmoja ana upanga wake mkononi,
tayari kumkabili adui usiku.
9Mfalme Solomoni alijitengenezea machela,
kwa mbao nzuri kutoka Lebanoni.
10Nguzo zake zilitengenezwa kwa fedha;
mgongo wake kwa dhahabu;
mahali pa kukalia pamefunikwa vitambaa vya zambarau,
walichoshona kwa upendo wanawake wa Yerusalemu,
waliokishonea alama za upendo.
11Njoni basi enyi wanawake wa Siyoni,
mkamwone mfalme Solomoni.
Amevalia taji aliyovikwa na mama yake,
siku alipofanya harusi yake,
naam, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.

Iliyochaguliwa sasa

Wimbo Ulio Bora 3: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia