Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 93

93
Mungu mfalme
1Mwenyezi-Mungu anatawala;
amejivika fahari kuu!
Mwenyezi-Mungu amevaa fahari na nguvu!
Ameuimarisha ulimwengu, nao hautatikisika kamwe.
2Kiti chako cha enzi ni imara tangu kale;
wewe umekuwapo kabla ya nyakati zote.
3Vilindi vimetoa sauti, ee Mwenyezi-Mungu;
naam, vimepaza sauti yake,
vilindi vyapaza tena mvumo wake.
4Mwenyezi-Mungu ana enzi kuu juu mbinguni,
ana nguvu kuliko mlio wa bahari,
ana nguvu kuliko mawimbi ya maji.
5Ee Mwenyezi-Mungu, maagizo yako ni thabiti;
nyumba yako ni takatifu milele na milele.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 93: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia