Zaburi 7:1-5
Zaburi 7:1-5 BHN
Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, nakimbilia usalama kwako; uniokoe na wote wanaonidhulumu, unisalimishe. La sivyo, watakuja kunirarua kama simba, wakanivutia mbali, pasiwe na wa kuniokoa. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu! Kama nimetenda moja ya mambo haya: Kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya, kama nimemlipa rafiki yangu mabaya badala ya mema, au nimemshambulia adui yangu bila sababu, basi, adui na anifuatie na kunikamata; ayakanyage maisha yangu; na kuniulia mbali.