Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 38:6-10

Zaburi 38:6-10 BHN

Nimepindika mpaka chini na kupondeka; mchana kutwa nazunguka nikiomboleza. Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa; mwilini mwangu hamna nafuu yoyote. Nimelegea na kupondekapondeka; nasononeka kwa kusongwa moyoni. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote; kwako hakikufichika kilio changu. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia; hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.

Soma Zaburi 38