Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 38:6-10

Zab 38:6-10 SUV

Nimepindika na kuinama sana, Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika. Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu. Nimedhoofika na kuchubuka sana, Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu. Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako. Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.