Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 27

27
Kwa Mungu kuna usalama
(Zaburi ya Daudi)
1Mwenyezi-Mungu ni mwanga wangu na wokovu wangu,
ni nani nitakayemwogopa?
Mwenyezi-Mungu ni ngome ya maisha yangu,
sitamwogopa mtu yeyote.
2Waovu wakinishambulia,
na kutaka kuniangamiza,
hao wapinzani wangu watajikwaa na kuanguka.
3Hata jeshi likinizunguka,
moyo wangu hautaogopa kitu;
hata nikikabiliwa na vita,
bado nitakuwa na tumaini.
4Jambo moja nimemwomba Mwenyezi-Mungu,
nalo ndilo ninalolitafuta:
Nikae nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu
siku zote za maisha yangu;
niuone uzuri wake Mwenyezi-Mungu,
na kutafuta maongozi yake hekaluni mwake.
5Siku ya taabu atanificha bandani mwake;
atanificha katika hema lake,
na kunisalimisha juu ya mwamba.
6Nami kwa fahari nitaangalia juu
ya maadui zangu wanaonizunguka.
Nitamtolea tambiko kwa shangwe hekaluni mwake,
nitaimba na kumshangilia Mwenyezi-Mungu.
Msaada wapatikana kwa Mungu
7Usikie, ee Mwenyezi-Mungu, ninapokulilia,
unionee huruma na kunijibu.
8Moyo wangu waniambia: “Njoo umtafute Mungu!”#27:8 Njoo umtafute Mungu: Kiebrania: Utafute uso wangu, yaani kumwendea Mungu katika ibada na kumtegemea (taz pia 2Sam 21:1).
Basi, naja kwako, ee Mwenyezi-Mungu.
9Usiache kuniangalia kwa wema.
Usinikatae kwa hasira mimi mtumishi wako;
wewe umekuwa daima msaada wangu.
Usinitupe wala usiniache, ee Mungu Mwokozi wangu.
10Hata kama wazazi wangu wakinitupa,
Mwenyezi-Mungu atanipokea kwake.
11Unifundishe njia yako, ee Mwenyezi-Mungu;
uniongoze katika njia iliyo sawa,
kwa sababu ya maadui zangu.
12Usiniache maadui wanitende wapendavyo;
maana mashahidi wa uongo wananikabili,
nao wanatoa vitisho vya ukatili.
13Naamini nitauona wema wake Mwenyezi-Mungu
katika makao ya walio hai.
14Mtegemee Mwenyezi-Mungu!
Uwe na moyo, usikate tamaa!
Naam, mtegemee Mwenyezi-Mungu!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 27: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha