Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 144:1-15

Zaburi 144:1-15 BHN

Atukuzwe Mwenyezi-Mungu, mwamba wangu, anayeipa mikono yangu mazoezi ya vita, na kuvifunza vidole vyangu kupigana. Yeye ni rafiki yangu amini na ngome yangu, kinga yangu na mkombozi wangu; yeye ni ngao yangu, kwake napata usalama; huyashinda mataifa na kuyaweka chini yangu. Ee Mwenyezi-Mungu, mtu ni nini hata umjali? Mwanadamu ni nini hata umfikirie? Binadamu ni kama pumzi tu; siku zake ni kama kivuli kipitacho. Uinamishe mbingu zako, ee Mwenyezi-Mungu, ushuke chini! Uiguse milima nayo itoe moshi! Lipusha umeme, uwatawanye maadui; upige mishale yako, uwakimbize! Unyoshe mkono wako kutoka juu, uniokoe na kuniondoa katika maji haya mengi; uniondoe makuchani mwa wageni, ambao husema maneno ya uongo, hunyosha mkono kushuhudia uongo. Nitakuimbia wimbo mpya, ee Mungu; nitakupigia kinubi cha nyuzi kumi, wewe uwapaye wafalme ushindi, umwokoaye Daudi mtumishi wako! Uniokoe na upanga wa adui katili, uniondoe makuchani mwa wageni, ambao husema maneno ya uongo, hunyosha mkono kushuhudia uongo. Wavulana wetu wakue kikamilifu kama mimea bustanini; binti zetu wawe kama nguzo zilizochongwa kupambia ikulu. Ghala zetu zijae mazao ya kila aina. Kondoo wetu mashambani wazae maelfu kwa maelfu. Mifugo yetu iwe na afya na nguvu; isitupe mimba wala kuzaa kabla ya wakati. Kusiwepo tena udhalimu mitaani mwetu. Heri taifa ambalo limejaliwa hayo! Heri taifa ambalo Mungu wao ni Mwenyezi-Mungu!

Soma Zaburi 144

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 144:1-15

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha