Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 144:1-15

Zaburi 144:1-15 SRUV

Na ahimidiwe BWANA, mwamba wangu, Aifundishaye mikono yangu vita, Na vidole vyangu kupigana. Mwamba wangu na ngome yangu, Nguzo yangu na mwokozi wangu Ngao yangu ninayemkimbilia, Huwatiisha watu wangu chini yangu. Ee BWANA, mtu ni kitu gani hata umjali? Na binadamu hata umwangalie? Binadamu ni kama ubatili, Siku zake ni kama kivuli kipitacho. Ee BWANA, uziinamishe mbingu zako, ushuke chini. Uiguse milima ili nayo itoe moshi. Utupe umeme, uwatawanye, Uipige mishale yako, uwafadhaishe. Uinyoshe mikono yako toka juu, uniponye, Unitoe katika maji mengi, kutoka kwa mkono wa wageni, Vinywa vyao vinasema visivyofaa, Na ambao mikono yao ya kulia ni ya uongo. Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, Kwa kinanda chenye nyuzi kumi nitakuimbia. Awapaye wafalme wokovu, Amwokoa Daudi, mtumishi wake, na upanga wa uovu. Uniponye, unitoe, Katika mkono wa wageni. Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao wa kulia ni mkono wa uongo. Wavulana wetu wakiwa ujanani wawe kama miche Iliyostawi kikamilifu. Binti zetu wawe kama nguzo za pembeni Zilizochongwa ili kupamba kasri. Ghala zetu na zijae Zenye akiba za jinsi zote. Kondoo zetu na wazae Elfu na makumi elfu mashambani mwetu. Ng'ombe wetu na wabebe mizigo mizito, Kusiwe na kushambuliwa. Wala kusiwe na kuhamishwa, Wala malalamiko katika njia zetu. Heri watu wenye hali hiyo, Heri watu wenye BWANA kuwa Mungu wao.

Soma Zaburi 144

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 144:1-15

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha