Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 61:1-4

Isaya 61:1-4 BHN

Bwana Mwenyezi-Mungu amenijaza roho yake, maana Mwenyezi-Mungu ameniweka wakfu, akanituma niwaletee wanaokandamizwa habari njema, niwatibu waliovunjika moyo, niwatangazie mateka kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa. Amenituma niutangaze mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi; niwafariji wote wanaoomboleza; niwape wale wanaoomboleza katika Siyoni taji la maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya moyo mzito. Nao wataitwa mialoni madhubuti, aliyopanda Mwenyezi-Mungu kuonesha utukufu wake. Watayajenga upya magofu ya zamani, wataisimika miji iliyoharibiwa hapo kwanza; wataitengeneza miji iliyobomolewa, uharibifu wa vizazi vingi vilivyopita.

Soma Isaya 61