Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Mambo ya Nyakati 1:35-54

1 Mambo ya Nyakati 1:35-54 BHN

Wana wa Esau walikuwa Elifazi, Reueli, Yeushi, Yalamu na Kora. Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Sefo, Gatamu, Kenazi, Timna na Amaleki. Wana wa Reueli walikuwa Nahathi, Zera, Shama na Miza. Wana wa Seiri walikuwa Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Eseri na Dishani. Wana wa Lotani walikuwa wawili: Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timna. Wana wa Shobali walikuwa Alvani, Manahathi, Ebali, Shefi na Onamu. Wana wa Sibeoni walikuwa Aya na Ana. Mwana wa Ana alikuwa Dishoni; na wana wa Dishoni walikuwa Hamrani, Eshbani, Ithrani na Kerani. Wana wa Eseri walikuwa Bilhani, Zaawani na Akani; na wana wa Dishoni walikuwa Usi na Arani. Wafuatao ndio wafalme waliotawala nchi ya Edomu kabla mfalme yeyote hajatawala Waisraeli: Bela mwana wa Beori alitawala nchi ya Edomu, akiwa na makao yake makuu katika mji wa Dinhaba. Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra alitawala badala yake. Yobabu alipofariki, Hushamu wa nchi ya Watemi alitawala badala yake. Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi alitawala badala yake, makao yake makuu yakiwa katika mji wa Avithi. Huyu ndiye aliyewapiga na kuwashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu. Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka alitawala badala yake. Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ulio karibu na mto Eufrate, alitawala badala yake. Shauli alipofariki, Baal-hanani mwana wa Akbori alitawala badala yake. Baal-hanani alipofariki, Hadadi kutoka Pai alitawala badala yake na jina la mkewe Akbori lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, binti Mezahabu. Naye Hadadi akafariki. Wakuu wa makabila ya Edomu walikuwa Timna, Alva, Yethethi, Oholibama, Ela, Pinoni, Kenazi, Temani, Mibsari, Magdieli na Iramu. Hao ndio wakuu wa makabila ya Edomu.