Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Sefania 3

3
Uovu wa Yerusalemu
1Ole wake yeye aliyeasi na kutiwa unajisi, mji wa udhalimu! 2#Yer 22:21; 5:3 Hakuitii sauti; hakukubali kurudiwa; hakumwamini BWANA; hakumkaribia Mungu wake. 3Wakuu wake walio ndani yake ni simba wangurumao; mahakimu wake ni mbwamwitu wa jioni; wasiobakiza kitu chochote mpaka asubuhi. 4#Yer 23:11; Eze 22:26 Manabii wake ni watu hafifu, wadanganyifu; makuhani wake wamepatia unajisi patakatifu, wameifanyia sheria udhalimu. 5#Kum 32:4; Zab 99:3,4 BWANA kati yake ni mwenye haki; hatatenda uovu; kila asubuhi hudhihirisha hukumu yake, wala hakomi; bali mtu asiye haki hajui kuona haya. 6Nimekatilia mbali mataifa, minara yao ina ukiwa; nimeziharibu njia kuu zao, hata hapana mmoja apitaye; miji yao imeangamizwa; hamna mtu hata mmoja, wala hapana akaaye huko. 7#Mwa 6:12 Nilisema, Hakika utaniogopa, utakubali kurudiwa; ili yasikatiliwe mbali makao yake, sawasawa ya yote niliyoagiza katika habari zake; lakini waliondoka mapema na kuyaharibu matendo yao yote.
Adhabu na wokovu wa mataifa
8 # Mit 20:22; Yoe 3:2 Basi ningojeeni, asema BWANA, hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.
9Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la BWANA, wamtumikie kwa nia moja. 10#Zab 68:31; Mal 1:11; Mdo 8:27 Maana toka nchi iliyo mbali na mito ya Kushi, waniombao dua, yaani, binti za watu wangu waliotawanyika, wataleta matoleo yangu. 11#Mt 3:9 Siku ile hutaaibishwa kwa matendo yako yote uliyoniasi; maana hapo nitawaondoa watu wako wanaojigamba na kujivuna, wasiwe kati yako, wala hutatakabari tena katika mlima wangu mtakatifu. 12#Isa 14:32; 57:15; Mt 5:3; Lk 6:20 Lakini nitabakiza ndani yako watu walioonewa na maskini, nao watalitumainia jina la BWANA. 13#Ufu 14:5 Mabaki ya Israeli hawatatenda uovu, wala kusema uongo; wala ulimi wa hadaa hautakuwa kinywani mwao; kwa maana watakula na kulala, wala hapana mtu atakayewatisha.
Wimbo wa shangwe
14 # Zab 14:7 Imba, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee Israeli;
Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti Yerusalemu.
15 # Yn 1:49; Eze 48:35; Ufu 21:3 BWANA ameziondoa hukumu zako,
Amemtupa nje adui yako;
Mfalme wa Israeli, naam, yeye BWANA, yuko katikati yako;
Hutaogopa uovu tena.
16 # Isa 35:3 Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa,
Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee.
17BWANA, Mungu wako, yuko katikati yako shujaa awezaye kuokoa;
Atakushangilia kwa furaha kuu,
Atakutuliza katika upendo wake,
Atakufurahia kwa kuimba.
18 # Omb 2:6 Nitawakusanya wanaousikitikia mkutano wa ibada, hao waliokuwa wa kwako; ambao mzigo uliokuwa juu yake ulikuwa fedheha kwao. 19Tazama, wakati huo nitawapatiliza watu wote wanaokutesa; nami nitamponya yeye achechemeaye, nami nitamkusanya yeye aliyefukuzwa; nami nitawafanya msifiwe na kujulikana, hao ambao aibu yao ilikuwa katika dunia yote. 20#Zab 22:27 Wakati huo nitawaingizeni, na wakati huo nitawakusanya; kwa maana nitawafanya ninyi msifiwe na mjulikane, miongoni mwa watu wote wa dunia, nitakapowarudisha wafungwa wenu mbele ya macho yenu, asema BWANA.

Iliyochaguliwa sasa

Sefania 3: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha