Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 9:1-20

Zaburi 9:1-20 SRUV

Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote; Nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu; Nitafurahi na kukushangilia; Nitaliimbia sifa jina lako, Wewe Uliye juu. Kwa sababu adui zangu hurudi nyuma; Hujikwaa na kuangamia mbele zako. Kwa maana umenifanyia hukumu na haki Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki. Umewakemea mataifa; Na kumwangamiza mdhalimu; Umelifuta jina lao milele na milele; Adui wameangamia na kuwa magofu milele. Nayo miji yao uliing'oa; Hata kumbukumbu lao limepotea. Bali BWANA atakaa milele, Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu. Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki; Atawaamua watu kwa uadilifu. BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida. Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, Maana Wewe, BWANA hukuwaacha wakutafutao. Mwimbieni BWANA akaaye Sayuni, Yatangazeni kwa watu matendo yake. Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka, Hakukisahau kilio cha wanyonge. Wewe, BWANA, unifadhili, Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia; Wewe uniinuaye katika malango ya mauti, Ili nizisimulie sifa zako zote; Katika malango ya binti Sayuni Nitaufurahia wokovu wako. Mataifa wamezama katika shimo walilolichimba; Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao. BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake. Wadhalimu wataenda kuzimu, Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu. Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima; Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele. Inuka, ee BWANA, mwanadamu asipate nguvu, Mataifa wahukumiwe mbele zako. Uwatie hofu, ee BWANA, Watu wa mataifa na wajitambue kuwa wao ni binadamu tu!

Soma Zaburi 9

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 9:1-20

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha