Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 71:1-24

Zaburi 71:1-24 SRUV

Nimekukimbilia Wewe, BWANA, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye, uniponye, Unitegee sikio lako, uniokoe. Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, Ngome imara ya wokovu wangu. Maana wewe, Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu. Ee Mungu wangu, uniponye mkononi mwa mkorofi, Katika mkono wake mwovu na mdhalimu, Maana ndiwe tegemeo langu, Ee Bwana MUNGU, Tumaini langu tokea ujana wangu. Nimekutegemea Wewe tangu kuzaliwa, Ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu, Ninakusifu Wewe daima. Nimekuwa kifani kwa watu wengi, Lakini wewe ndiwe kimbilio langu la nguvu. Kinywa changu kitajazwa sifa zako, Na heshima yako mchana kutwa. Usinitupe wakati wa uzee, Nguvu zangu zipungukapo usiniache. Kwa maana adui zangu wananiamba, Nao wanaotaka kuniua hushauriana. Wakisema, Mungu amemwacha, Mfuatieni, mkamateni, hakuna wa kumponya. Ee Mungu, usiwe mbali nami; Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia. Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya. Lakini mimi nitakutumainia daima, Nitaendelea kukusifu zaidi na zaidi. Lakini mimi nitakutumainia daima Na nitaendelea kukusifu zaidi na zaidi. Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako. Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo. Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako. Na haki yako, Ee Mungu, Imefika juu sana. Wewe uliyefanya mambo makuu; Ee Mungu, ni nani aliye kama Wewe? Wewe, uliyetuonesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Kutoka katika vina virefu chini ya nchi. Laiti ungeniongezea ukuu! Urejee tena na kunifariji moyo. Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu. Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli. Midomo yangu itafurahi sana nikuimbiapo, Na nafsi yangu uliyoikomboa. Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya.

Soma Zaburi 71

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha