Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 51

51
Sala ya utakaso na msamaha
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi, wakati Nabii Nathani alipomjia, alipokuwa amekwisha kwenda kwa Bathsheba
1 # Kol 2:14 Ee Mungu, unirehemu,
kulingana na fadhili zako.
Kiasi cha wingi wa rehema zako,
Uyafute makosa yangu.
2 # Eze 36:25; Zek 13:1; 1 Kor 6:11; Ebr 9:14; 1 Yoh 1:7; Ufu 1:5 Unioshe kabisa uovu wangu,
Unitakase dhambi zangu.
3 # Zab 32:5 Maana nimejua mimi makosa yangu
Na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 # Rum 3:4; Lk 15:21; Mwa 39:9 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,
Na kufanya maovu mbele za macho yako.
Wewe ujulikane kuwa una haki unenapo,
Na kuwa safi utoapo hukumu.
5 # Ayu 14:4; Yn 3:6; Rum 5:12 Tazama, nikazaliwa nikiwa na hatia;
Mama yangu akanichukua mimba nikiwa na dhambi.
6Tazama, wapendezwa na kweli iliyo moyoni;
Nawe utanifundisha hekima kwa siri,
7Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,
Unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8Unifanye kusikia furaha na shangwe,
Mifupa uliyoiponda ifurahi.
9Usitiri uso wako usitazame dhambi zangu;
Uzifute hatia zangu zote.
10 # Mit 20:9; Yer 13:27; Eze 11:19; Mdo 15:9; Efe 2:10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi,
Uifanye upya na kuithibiti roho yangu.
11 # Mwa 4:14; Eze 36:27; Rum 8:9 Usinitenge na uso wako,
Wala roho yako mtakatifu usiniondolee.
12 # Rum 8:15; 2 Kor 3:17 Unirudishie furaha ya wokovu wako;
Unitegemeze kwa roho ya upendo.
13Nitawafundisha wakosaji njia zako,
Na wenye dhambi watarejea kwako.
14Ee MUNGU, Mungu wa wokovu wangu,
Uniponye na umwagaji wa damu,
Na ulimi wangu utaiimba haki yako.
15Ee Bwana, uifumbue midomo yangu,
Na kinywa changu kitazinena sifa zako.
16Maana hupendezwi na dhabihu, na kama ningeitoa,
Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.
17Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika;
Moyo uliovunjika na kupondeka,
Ee Mungu, hutaudharau.
18Uitendee mema Sayuni kwa radhi yako,
Uzijenge kuta za Yerusalemu.
19 # Mal 3:3 Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za haki,
Na sadaka za kuteketezwa, na kafara.
Ndipo watakapotoa ng'ombe
Juu ya madhabahu yako.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 51: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha