Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 39

39
Sala ya kutaka hekima na msamaha
Kwa mwimbishaji: kwa Yeduthuni. Zaburi ya Daudi.
1 # 1 Fal 2:4; Mit 4:26,27; Ebr 2:1; Kol 4:5 Nilisema, Nitazitunza njia zangu
Nisije nikakosa kwa ulimi wangu;
Nitajitia lijamu kinywani,
Maadamu mtu mbaya awapo mbele yangu.
2Nilikuwa sisemi, nilinyamaa kimya,
Sina faraja, maumivu yangu yakazidi.
3 # Yer 20:9 Moyo wangu ukawa moto ndani yangu,
Na katika kuwaza kwangu moto ukawaka;
Nilisema kwa ulimi wangu,
4BWANA, unijulishe mwisho wangu,
Na idadi ya siku zangu ni ngapi;
Nijue jinsi maisha yangu yalivyo mafupi.
5 # Zab 90:4 Tazama, umefanya siku zangu kuwa mashubiri;
Maisha yangu ni kama si kitu mbele zako.
Kila mwanadamu, ingawa amesitawi, ni ubatili.
6Kweli, watu wote hupita kama kivuli;
Wao hujisumbua bure tu;
Wanajirundikia mali wala hawajui ni nani atakayeirithi.
7Na sasa ninangoja nini, Ee Bwana?
Matumaini yangu ni kwako.
8Uniokoe kutoka kwa maasi yangu yote,
Usinifanye niwe wa kulaumiwa na mpumbavu.
9Nimenyamaza, sifumbui kinywa changu,
Maana Wewe ndiwe uliyeyafanya.
10Uniondolee pigo lako;
Kwa mapigo ya mkono wako nimeangamia.
11Ukimrudi mtu kwa kumkemea kwa uovu wake,
Watowesha uzuri wake kama nondo.
Kila mwanadamu ni ubatili.
12 # Law 25:23; 1 Nya 29:15 Ee BWANA, usikie maombi yangu,
Utege sikio lako niliapo,
Usiyapuuze machozi yangu.
Kwa maana mimi ni mgeni wako,
Msafiri kama baba zangu wote.
13 # Ayu 10:20,21 Uache kunitazama, ndio nipate kufurahi tena,
Kabla sijafa na kutoweka kabisa.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 39: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha