Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 27:7-14

Zaburi 27:7-14 SRUV

Ee BWANA, usikie, kwa sauti yangu ninalia, Unifadhili, unijibu. Uliposema, “Nitafuteni uso wangu,” Moyo wangu umekuambia, BWANA, uso wako nitautafuta. Usinifiche uso wako, Usimkatalie mtumishi wako kwa hasira. Umekuwa msaada wangu, usinitupe, Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu. Hata baba yangu na mama yangu wakiniacha, Bali BWANA atanikaribisha kwake. Ee BWANA, unifundishe njia yako, Na kuniongoza katika njia iliyonyoka; Kwa sababu yao wanaoniotea; Usinitie katika nia ya watesi wangu; Maana mashahidi wa uongo wamenijia, Nao watoao jeuri kama pumzi. Naamini ya kuwa nitauona wema wa BWANA Katika nchi ya walio hai. Umtumainie BWANA, uwe imara, Upige moyo konde, naam, umngoje BWANA.

Soma Zaburi 27

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 27:7-14