Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 142

142
Sala ya ukombozi kutoka kwa watesi
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Ombi.
1 # 1 Sam 22:1; 24:3 Kwa sauti yangu nitamlilia BWANA,
Kwa sauti yangu nitamwomba BWANA dua.
2Nitafunua mbele zake malalamiko yangu,
Shida yangu nitaitangaza mbele zake.
3Roho yangu inapozimia unayajua mapito yangu;
Katika njia niendayo wamenifichia mtego.
4Utazame mkono wangu wa kulia ukaone,
Kwa maana sina mtu anijuaye.
Makimbilio yamenipotea,
Hakuna wa kunitunza roho.
5 # Omb 3:24 BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu,
Fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 # Zab 116:6; 7:1 Ukisikilize kilio changu,
Kwa maana nimedhilika sana.
Uniponye kutoka kwa wanaonifuatia,
Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.
7 # Zab 34:2; 119:17 Uitoe nafsi yangu kifungoni.
Nipate kulishukuru jina lako.
Wenye haki watanizunguka,
Kwa kuwa Wewe unanikirimu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 142: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha