Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 141

141
Sala ya kutaka kulindwa kutoka kwenye uovu
1Ee BWANA, nimekuita, unijie hima,
Uisikie sauti yangu nikuitapo.
2 # Efe 5:2; 1 Tim 2:8; Ufu 5:8 Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba,
Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.
3Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu,
Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.
4 # Mt 6:14; 20:15; Mit 23:6 Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya,
Nisiyazoelee matendo yasiyofaa,
Pamoja na watu watendao maovu;
Wala nisile vyakula vyao vya anasa.
5Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili;
Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani;
Kichwa changu kisikatae,
Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.
6Wakuu wao wakiangushwa kando ya genge,
Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.
7 # 2 Kor 1:9 Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi,
Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.
8 # Zab 25:15 Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana,
Nimekukimbilia Wewe, usiniache bila kinga.
9Unilinde kutoka kwa mtego walionitegea,
Na kutoka kwa matanzi ya watendao maovu.
10 # Est 7:10; Zab 7:15 Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe,
Wakati ninapopita salama.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 141: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha