Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 128

128
Nyumba ya mwumini yenye furaha
Wimbo wa kupanda mlima.
1Heri kila mtu amchaye BWANA,
Aendaye katika njia yake.
2 # Isa 3:10 Taabu ya mikono yako hakika utaila;
Utakuwa heri, na kwako kwema.
3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,
Katika nyumba yako.
Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni
Wakiizunguka meza yako.
4Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.
5 # Zab 134:3 BWANA akubariki toka Sayuni;
Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;
6 # Mwa 50:23 Naam, ukawaone wana wa wanao.
Amani ikae na Israeli.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 128: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha