Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:33-40

Zaburi 119:33-40 SRUV

Ee BWANA, unifundishe njia ya amri zako, Nami nitaishika hadi mwisho. Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote. Uniendeshe katika mapito ya amri zako, Kwa maana nimependezwa nayo. Unielekeze moyo wangu katika shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa. Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako. Umthibitishie mtumishi wako ahadi yako, Iliyo ya wanaokucha. Uniondolee laumu niiogopayo, Maana hukumu zako ni njema. Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.

Soma Zaburi 119