Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 119:33-40

Zaburi 119:33-40 NEN

Ee BWANA, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho. Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote. Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha. Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi. Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako. Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa. Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema. Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha