Mithali 27:23-27
Mithali 27:23-27 SRUV
Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako; Na kuwaangalia sana ng'ombe wako. Kwa maana mali haziwi za milele; Na taji je! Ladumu tangu kizazi hata kizazi? Manyasi hukatwa, na majani mabichi huchipua, Na mboga ya mlimani hukusanywa. Wana-kondoo hufaa kwa mavazi yako; Na mbuzi ni thamani ya shamba. Tena yatakuwapo maziwa ya mbuzi, Ya kukutosha kwa chakula chako, Na chakula cha watu wa nyumbani mwako, Na posho la vijakazi vyako.