Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 12

12
1Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa;
Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
2Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;
Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
3Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;
Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
4 # Mit 31:23; 1 Kor 11:7; Mit 14:30 Mwanamke mwema ni taji la mumewe;
Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5Mawazo ya mwenye haki ni adili;
Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6Maneno ya waovu huotea damu;
Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7 # Mt 7:24 Waovu huangamia, hata hawako tena;
Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8 # 1 Sam 13:13; Mal 2:8,9; Mit 1:25,26; 3:35; Mt 27:4,5 Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;
Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,
Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10 # Kum 25:4 Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;
Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11 # Mwa 3:19; Mit 28:19; Efe 4:28; 1 The 4:11 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;
Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12 # Zab 1:3; Lk 8:15 Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;
Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13 # 2 Pet 2:9 Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;
Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14 # Isa 3:10 Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;
Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
15 # Lk 18:11 Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe;
Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16Ghadhabu ya mpumbavu hujulikana mara;
Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
17Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki;
Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
18Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;
Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19 # Zek 1:5,6 Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;
Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
20Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;
Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21 # Rum 8:28; 2 The 1:6; 2 Pet 2:9 Mwenye haki hatapatikana na msiba wowote;
Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22 # Ufu 22:15 Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA;
Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa;
Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
24 # 1 Fal 11:28; Mit 10:4 Mkono wa mwenye bidii utatawala;
Bali mvivu atalipishwa kodi.
25 # Isa 50:4 Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha;
Bali neno jema huufurahisha.
26Mwenye haki ni kiongozi wa mwenzake;
Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
27Mtu mvivu hapiki mawindo yake;
Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.
28 # Kum 30:15; Mt 19:17; Rum 5:21; 2 Kor 4:17; Ufu 2:7 Katika njia ya haki kuna uhai;
Wala hakuna mauti katika mapito yake.

Iliyochaguliwa sasa

Mithali 12: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha