Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 11

11
1Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa BWANA;
Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza.
2 # Dan 4:30 Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu;
Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.
3Ukamilifu wao wenye haki utawaongoza
Bali ukaidi wao wenye fitina utawaangamiza.
4 # Eze 7:19; Sef 1:18; Mwa 7:1 Mali hazifaidii kitu siku ya ghadhabu;
Bali haki huokoa na mauti.
5Haki yake mtu mkamilifu itamwongoza njia yake;
Bali mtu mwovu ataanguka kwa uovu wake.
6 # 1 Tim 4:8; Mhu 10:8 Haki yao wenye haki itawaokoa;
Bali wafanyao fitina watanaswa kwa hila yao wenyewe.
7Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake linapotea;
Na matumaini ya uovu huangamia.
8Mwenye haki huokolewa katika dhiki,
Na mtu mwovu ataiingia badala yake.
9 # Ayu 8:13 Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;
Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
10 # Est 8:15 Wenye haki wasitawipo, mji hufurahi;
Waovu wanapoangamia, watu hushangilia.
11Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki;
Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.
12Asiye na akili humdharau mwenziwe;
Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.
13Mwenye udaku hupitapita akifunua siri;
Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.
14 # 1 Fal 12:1 Pasipo mashauri taifa huanguka;
Bali kwa wingi wa washauri huja wokovu.
15Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;
Achukiaye mambo ya dhamana yuko salama.
16Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima;
Na watu wakali hushika mali siku zote.
17 # Mt 25:34 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake;
Aliye mkali hujisumbua mwili wake.
18 # Hos 10:12; Gal 6:8,9 Mtu mwovu hupata mshahara wa udanganyifu;
Apandaye haki ana thawabu ya hakika.
19Haki huelekea uzima;
Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.
20Wenye uhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA;
Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.
21Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu;
Bali wazawa wa wenye haki wataokoka.
22Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe,
Ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na akili.
23 # Rum 2:8 Haja ya mwenye haki ni kupata mema tu;
Bali kutaraji kwake mtu mwovu huishia katika ghadhabu.
24Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi;
Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji.
25 # Mt 5:7 Nafsi ya mtu mkarimu itastawishwa;
Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.
26 # Amo 8:5; Ayu 29:13 Awanyimaye watu nafaka, watu watamlaani;
Auzaye nafaka, baraka itakuwa kichwani pake.
27 # Est 7:10 Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili;
Atafutaye madhara, hayo yatamjia.
28 # Mk 10:24; Lk 12:21; 1 Tim 6:17; Yer 17:8 Azitegemeaye mali zake ataanguka;
Mwenye haki atasitawi kama jani.
29 # Mhu 5:16 Ataabishaye nyumba yake mwenyewe ataurithi upepo;
Mpumbavu atakuwa mtumwa wa mtu mwenye moyo wa akili.
30Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima;
Na mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 # 1 Pet 4:18; Yer 25:29 Ikiwa, mwenye haki atalipwa duniani;
Je, mwovu na mkosaji hawatalipwa mara nyingi zaidi?

Iliyochaguliwa sasa

Mithali 11: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha