Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hesabu 10:29-36

Hesabu 10:29-36 SRUV

Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo BWANA amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa BWANA ametamka mema juu ya Israeli. Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe. Naye akamwambia, Usituache, tafadhali; kwa kuwa wewe wajua jinsi tutakavyopiga kambi, nawe utakuwa kiongozi wetu. Isitoshe, ukienda pamoja nasi, naam, mema yote ambayo BWANA atatutendea, nawe tutakutendea vivyo hivyo. Basi wakasafiri kutoka penye mlima wa BWANA safari ya siku tatu; na sanduku la Agano la BWANA likatangulia mbele yao mwendo wa siku tatu, ili kuwatafutia mahali pa kupumzika. Na wingu la BWANA lilikuwa juu yao mchana hapo waliposafiri kwenda mbele kutoka kambini. Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee BWANA, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao. Tena hapo liliposimama, akasema, Ee BWANA, uwarudie maelfu kumi ya maelfu ya Israeli.

Soma Hesabu 10

Video for Hesabu 10:29-36