Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 38:1-18

Ayubu 38:1-18 SRUV

Ndipo BWANA akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema, Ni nani huyu atiaye ushauri giza Kwa maneno yasiyo na maarifa? Basi jifunge viuno kama mwanamume, Maana nitakuuliza neno, nawe niambie. Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama una ufahamu. Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake – hakika unajua! Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake? Misingi yake ilikazwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni, Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha? Au ni nani aliyeifunga bahari kwa milango, Hapo ilipotoka kwa nguvu kama kwamba imetoka tumboni mwa nchi. Nilipolifanya wingu kuwa vazi lake, Na giza zito kuwa nguo ya kuifungia, Nikaiagiza amri yangu; Nikaiwekea makomeo na milango, Nikasema, Utafika mpaka hapa, lakini hutapita, Na hapa mawimbi yako yenye nguvu yatazuiliwa? Je! Umeiamuru asubuhi tangu siku zako zilipoanza? Umeyajulisha mapambazuko mahali pake? Yapate kuishika miisho ya nchi, Waovu wakung'utwe wakawe mbali nayo? Hubadilika mfano wa udongo chini ya mhuri, Vitu vyote vinatokea kama mavazi. Na waovu nuru yao huzuiliwa isiwafikie, Na mkono ulioinuka huvunjika. Je! Umeziingia chemchemi za bahari, Au umetembea mahali pa siri pa vilindi? Je! Umefunuliwa malango ya mauti, Au umeyaona malango ya kuzimu? Umeyafahamu mapana ya dunia? Haya! Sema, ikiwa unayajua hayo yote.

Soma Ayubu 38

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Ayubu 38:1-18