Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hagai 2:20-23

Hagai 2:20-23 SRUV

Kisha neno la BWANA likamjia Hagai mara ya pili, siku ya ishirini na nne ya mwezi, kusema, Sema na Zerubabeli, mtawala wa Yuda, ukisema, Nitazitikisa mbingu na dunia; nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake. Katika siku ile, asema BWANA wa majeshi, nitakutwaa wewe, Ee Zerubabeli, mtumishi wangu, mwana wa Shealtieli, asema BWANA, nami nitakufanya kuwa kama pete yenye mhuri; kwa kuwa nimekuchagua, asema BWANA wa majeshi.

Soma Hagai 2

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Hagai 2:20-23