Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 28:31-39

Kutoka 28:31-39 SRUV

Nawe fanya hiyo joho la naivera ya rangi ya buluu yote. Nayo itakuwa na tundu katikati yake kwa kupitisha kichwa; itakuwa na utepe wa kazi ya kusokotwa kuzunguka hilo tundu lake, mfano wa tundu lililo katika kanzu ya chuma, ili lisipasuke. Nawe katika pindo zake utatia makomamanga ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, kuzunguka pindo zake kotekote; na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga pande zote; njuga ya dhahabu na komamanga, katika pindo za joho kuizunguka pande zote. Nayo itakuwa juu ya Haruni akitumika; na sauti ya hizo njuga itasikika hapo aingiapo ndani ya mahali patakatifu mbele ya BWANA na hapo atokapo nje, ili kwamba asife. Nawe fanya bamba la dhahabu safi na kuchora juu yake, mfano wa michoro ya mihuri, MTAKATIFU KWA BWANA. Nawe ulitie hilo bamba katika ukanda wa rangi ya buluu, nalo litakuwa katika kile kilemba; litakuwa upande wa mbele wa kile kilemba. Nalo litakuwa katika kipaji cha uso cha Haruni, na Haruni atauchukua uovu wa vile vitu vitakatifu, watakavyovitakasa hao wana wa Israeli katika vipawa vyao vyote vitakatifu, nalo litakuwa katika kipaji chake cha uso sikuzote, ili vipate kukubaliwa mbele za BWANA. Na hiyo kanzu utaifuma ya kitani nzuri ya kazi ya urembo, ufanye na kilemba cha nguo ya kitani nzuri, nawe utafanya mshipi wenye kunakishiwa vizuri.

Soma Kutoka 28