Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Samweli 22

22
Wimbo wa Shukrani wa Daudi
1 # Kut 15:1 Basi Daudi akamwambia BWANA maneno ya wimbo huu, siku ile BWANA alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na mkononi mwa Sauli; 2#Mwa 15:1; Kum 32:4; 1 Sam 2:2; Zab 18:2; 91:2; Mit 18:10; Mt 18:11 akasema,
BWANA ndiye jabali langu, na ngome yangu, na mwokozi wangu,
3 # Ebr 2:13; Mwa 15:1; Zab 3:3; Mit 30:5; Lk 1:69; Mit 18:10; Zab 9:9; 18:2; Isa 32:2; Isa 32:2; Yer 16:19 Mungu wa mwamba wangu, nitamwamini yeye;
Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, mnara wangu, na
kimbilio langu;
Mwokozi wangu, waniokoa na jeuri.
4Nitamwita BWANA astahiliye kusifiwa;
Hivyo nitaokoka na adui zangu.
5Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka,
Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
6Kamba za kuzimu zilinizunguka;
Mitego ya mauti ikanikabili.
7 # Zab 116:4; Yon 2:2; Kut 3:7 Katika shida yangu nilimwita BWANA,
Naam, nikamlalamikia Mungu wangu;
Naye akaisikia sauti yangu hekaluni mwake,
Kilio changu kikaingia masikioni mwake.
8 # Amu 5:4; Ayu 26:11; Zab 18:7; 77:18 Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka,
Misingi ya mbinguni ikasukasuka
Na kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.
9 # Zab 97:3; Hab 3:5; Ebr 12:29 Kukapanda moshi kutoka puani mwake,
Moto ukatoka kinywani mwake ukala;
Makaa yakawashwa nao.
10 # Isa 64:1 Aliziinamisha mbingu akashuka;
Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
11 # Zab 104:3 Akapanda juu ya kerubi akaruka;
Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.
12Akafanya giza hema zake za kumzunguka,
Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.
13Toka mwangaza uliokuwa mbele zake
Makaa ya moto yakawashwa.
14 # Isa 30:30 BWANA alipiga radi toka mbinguni,
Naye Aliye Juu akaitoa sauti yake.
15 # Kum 32:23; Zab 7:13; 77:17; Hab 3:11 Akapiga mishale, akawatawanya;
Umeme, naye akawatimua.
16Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari,
Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,
Kwa kukemea kwake BWANA,
Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.
17Alipeleka kutoka juu, akanishika;
Akanitoa katika maji mengi;
18Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,
Na wale walionichukia;
Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
19Walinikabili siku ya msiba wangu;
Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.
20 # Zab 31:8; 2 Sam 15:26 Akanitoa akanipeleka panapo nafasi;
Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
21BWANA alinitendea kulingana na haki yangu;
Kulingana na usafi wa mikono yangu akanilipa.
22Maana nimezishika njia za BWANA,
Wala sikumwasi Mungu wangu.
23 # Kum 7:12 Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu;
Na kuhusu amri zake, sikuziacha.
24 # Mwa 6:9; Ayu 1:1; Yn 1:47 Nami nilikuwa mkamilifu kwake,
Nikajilinda na uovu wangu.
25Basi BWANA amenilipa kulingana na haki yangu;
Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele zake.
26 # Mt 5:7 Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili
Kwa mkamilifu utajionesha kuwa mkamilifu;
27 # Law 26:23 Kwake ajitakasaye utajionesha kuwa mtakatifu;
Na kwa mpotovu utajionesha kuwa mkaidi.
28 # Kut 3:7; Zab 12:5; Mt 5:3 Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa;
Ila macho yako huwapinga wenye kiburi, uwadhili.
29Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee BWANA;
Na BWANA ataniangazia giza langu.
30Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi;
Kwa msaada wa Mungu wangu ninaruka ukuta.
31 # Kum 32:4; Dan 4:37; Ufu 15:3; Zab 12:6; Mit 30:5 Mungu njia yake ni kamilifu;
Ahadi ya BWANA imehakikishwa;
Yeye ndiye ngao yao
Wote wanaomkimbilia.
32 # Kum 32:31; 1 Sam 2:2; Isa 45:5,6 Maana ni nani aliye Mungu, ila BWANA?
Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?
33 # Zab 27:1; Kum 18:13 Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu;
Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.
34 # Hab 3:19 Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;
Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
35Ananifundisha mikono yangu vita;
Hata mikono yangu inaupanda upinde wa shaba.
36Nawe umenipa ngao ya wokovu wako;
Na unyenyekevu wako umenikuza.
37Umezifanyia nafasi hatua zangu,
Wala miguu yangu haikuteleza.
38Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza;
Wala sikurudi nyuma hadi walipokomeshwa.
39Nami nimewakomesha na kuwapiga wasiweze kusimama;
Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.
40Maana umenijaza nguvu ya kupigana vita;
Ukawafanya adui zangu wafifie chini yangu.
41Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,
Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
42 # 1 Sam 28:6; Ayu 27:9; Mit 1:28 Walitazama, lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;
Walimwita BWANA, lakini hakuwajibu.
43Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,
Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
44 # Kum 28:13; Isa 55:5 Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu;
Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa;
Watu nisiowajua watanitumikia.
45Wageni walinijia wakinyenyekea;
Mara tu waliposikia habari zangu,
Walinitii.
46 # Mik 7:17 Wageni nao waliishiwa nguvu,
Wakatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 # Zab 89:26 BWANA yu hai;
Na ahimidiwe mwamba wangu;
Na atukuzwe Mungu wangu, mwamba wa wokovu wangu;
48 # Zab 144:2 Naam, Mungu anilipiziaye kisasi,
Na kuwatweza watu chini yangu,
49Na kuniokoa kutoka kwa adui zangu;
Naam, waniinua juu yao walioniinukia;
Ukaniokoa kutoka kwa watu wajeuri.
50 # Rum 15:9 Basi, BWANA, nitakushukuru kati ya mataifa,
Nami nitaliimbia jina lako.
51Yeye ni mnara wa wokovu#22:51 Au wokovu mkuu. kwa mfalme wake;
Amfanyia fadhili masihi#22:51 Au, mtiwa mafuta (tazama 1 Sam 2:10). wake,
Kwa Daudi na wazawa wake, hata milele.

Iliyochaguliwa sasa

2 Samweli 22: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha