2 Wakorintho 13:5-9
2 Wakorintho 13:5-9 SRUV
Jichunguzeni wenyewe muone kama mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa iwe mmekataliwa. Lakini natumaini kama mtajua ya kuwa sisi hatukukataliwa. Nasi tunamwomba Mungu, msifanye lolote lililo baya; si kwamba sisi tuonekane tumekubaliwa, lakini ninyi mfanye lile lililo jema, ijapokuwa sisi tu kama waliokataliwa. Maana hatuwezi kutenda neno lolote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli. Maana twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa hodari. Tena twaomba hili nalo, kutimilika kwenu.