Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Wakorintho 4:14-21

1 Wakorintho 4:14-21 SRUV

Siyaandiki hayo ili kuwatahayarisha; bali kuwaonya kama watoto niwapendao. Kwa kuwa ijapokuwa mna waalimu elfu kumi katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili. Basi, nawasihi mnifuate mimi. Kwa sababu hii nimemtuma Timotheo kwenu, aliye mwanangu mpendwa, mwaminifu katika Bwana, atakayewakumbusha njia zangu zilizo katika Kristo, kama vile nifundishavyo kila mahali katika kila kanisa. Basi wengine wamejivuna kana kwamba siji kwenu. Lakini nitakuja kwenu upesi, nikijaliwa, nami nitafahamu, si neno lao tu wajivunao, bali nguvu zao. Maana ufalme wa Mungu hauwi katika neno, bali katika nguvu. Mnataka vipi? Nije kwenu na fimbo, au nije katika upendo na roho ya upole?