Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 97

97
Utukufu wa Enzi ya Mungu
1BWANA ametamalaki, nchi na ishangilie,
Visiwa vingi na vifurahi.
2Mawingu na giza vyamzunguka,
Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.
3 # Dan 7:10; Hab 3:5 Moto hutangulia mbele zake,
Nao huwateketeza watesi wake pande zote.
4Umeme wake uliuangaza ulimwengu,
Nchi ikaona ikatetemeka.
5Milima iliyeyuka kama nta mbele za BWANA,
Mbele za Bwana wa dunia yote.
6Mbingu zimetangaza haki yake,
Na watu wote wameuona utukufu wake.
7 # Kut 20:4; Law 26:1; Isa 37:18,19; Yer 10:14; Ebr 1:6 Na waaibishwe wote waabuduo sanamu,
Wajivunao kwa vitu visivyofaa;
Enyi miungu yote, msujuduni Yeye.
8Sayuni imesikia na kufurahi,
Binti za Yuda walishangilia,
Kwa sababu ya hukumu zako, Ee BWANA.
9 # Efe 1:21 Maana Wewe, BWANA, ndiwe Uliye juu,
Juu sana kuliko nchi yote;
Umetukuka sana juu ya miungu yote.
10 # Zab 101:3; Amo 5:15; Rum 7:15; 1 Sam 2:9; Mit 2:8; Dan 3:28 Enyi mmpendao BWANA, uchukieni uovu;
Huwalinda nafsi zao watauwa wake,
Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki.
11Nuru imemzukia mwenye haki,
Na furaha wanyofu wa moyo.
12Enyi wenye haki, mmfurahieni BWANA,
Na kulishukuru jina lake takatifu.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 97: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha