Mit 27:23-27
Mit 27:23-27 SUV
Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako; Na kuwaangalia sana ng’ombe zako. Kwa maana mali haziwi za milele; Na taji je! Yadumu tangu kizazi hata kizazi? Manyasi huchukuliwa, na majani mabichi huonekana, Na maboga ya milimani hukusanyika. Wana-kondoo hufaa kwa mavazi yako; Na mbuzi ni thamani ya shamba Tena yatakuwapo maziwa ya mbuzi, Ya kukutosha kwa chakula chako, Na chakula cha watu wa nyumbani mwako, Na posho la vijakazi vyako.